Timu ya volleyball ya
watoto wa kike kutoka shule ya msingi na sekondari MKALAPA Kata ya NDANDA iliyopo
Halmashauri ya Wilaya ya MASASI wameadhimisha siku ya wanawake duniani kwa mchezo
wa volleyball.
Wakizungumza baada ya
mchezo huo, wamefurahi na kuiomba jamii
kutoa kipaumbele katika michezo inayohusisha jinsia ya kike.
Ikumbukwe kuwa timu ya watoto hao ni moja kati
ya timu ambazo zimeupa ushindi Mkoa wa MTWARA katika mashindano ya UMISETA na UMITASHUMTA,
hivyo watoto wa kike wakiwezeshwa wanaweza katika kujitelea maendeleo na kushiriki katika safari ya kuelekea uchumi wa
Viwanda kwa kutumia vipaji vyao.
WAKATI HUOHUO
WAKATI HUOHUO
Halmashauri
ya Wilaya ya MASASI imeadhimisha siku ya Wanawake duniani katika Kata ya NDANDA
huku Mambo MATATU ya kumwezesha mwanamke ili kushiriki kwa vitendo kuelekea
uchumi wa viwanda ifikapo 2025 ikiwemo kuwawezesha kielimu, kuwapa mitaji na
kuwashirikisha katika maamuzi yakisisitizwa.
Halmashauri ya wilaya ya
Masasi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 jumla ya shilingi milioni 79,445,000
zimekopeshwa kwa vikundi 31 vya wanawake ikiwa ni mitaji ya kuendeleza biashara
zao na hivyo kuzalisha kwa tija ili kukuza uchumi wa kaya na Taifa kwa ujumla.
Kauli mbiu ya siku ya wanawake duniani mwaka 2018
unasema"KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA: TUIMARISHE USAWA WA KIJINSIA NA
UWEZESHAJI WANAWAKE VIJIJINI"
No comments:
Post a Comment