MASASI:wasichana waonyesha vipaji kwa kusakata "volleyball"


Image may contain: one or more people, people playing sports, sky, cloud, outdoor and natureTimu ya volleyball ya watoto wa kike kutoka shule ya msingi na sekondari MKALAPA Kata ya NDANDA iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya MASASI wameadhimisha siku ya wanawake duniani kwa mchezo wa volleyball.

Wakizungumza baada ya mchezo huo, wamefurahi  na kuiomba jamii kutoa kipaumbele katika michezo inayohusisha jinsia ya kike.

Ikumbukwe kuwa timu ya watoto hao ni moja kati ya timu ambazo zimeupa ushindi Mkoa wa MTWARA katika mashindano ya UMISETA na UMITASHUMTA, hivyo watoto wa kike wakiwezeshwa wanaweza katika kujitelea maendeleo na  kushiriki katika safari ya kuelekea uchumi wa Viwanda kwa kutumia vipaji vyao.


WAKATI HUOHUO

Image may contain: one or more people, people standing and textHalmashauri ya Wilaya ya MASASI imeadhimisha siku ya Wanawake duniani katika Kata ya NDANDA huku Mambo MATATU ya kumwezesha mwanamke ili kushiriki kwa vitendo kuelekea uchumi wa viwanda ifikapo 2025 ikiwemo kuwawezesha kielimu, kuwapa mitaji na kuwashirikisha katika maamuzi yakisisitizwa.

Image may contain: 7 people, people smiling, weddingHalmashauri ya wilaya ya Masasi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 jumla ya shilingi milioni 79,445,000 zimekopeshwa kwa vikundi 31 vya wanawake ikiwa ni mitaji ya kuendeleza biashara zao na hivyo kuzalisha kwa tija ili kukuza uchumi wa kaya na Taifa kwa ujumla.


Kauli mbiu ya siku ya wanawake duniani mwaka 2018 unasema"KUELEKEA UCHUMI WA VIWANDA: TUIMARISHE USAWA WA KIJINSIA NA UWEZESHAJI WANAWAKE VIJIJINI"

Share:

No comments:

SIKILIZA JAMII FM

Blog Archive

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

HABARI KUU WIKI HII

WAENDESHA BLOG

Contact Form



Recent post