Ikiwa leo Machi 8, 2018 ni kilele cha maadhimisho ya siku ya
wanawake duniani, Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Stadi, Profesa
Joyce Ndalichako na Spika Mstaafu wa Bunge, Anna Makinda wametoa somo kwa
wanawake hapa nchini.
Akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa
kuhusu masuala ya maendeleo endelevu ya Wanawake barani Afrika, Prof.
Ndalichako amewataka wanawake kufanya kazi kwa bidi ili waweze kuaminiwa na
jamii.
“Wito wangu ni kwamba tuendelee kufanya
kazi kwa bidii kwa sababu historia imemuweka mwanamke katika nafasi isiyo nzuri
kwa hiyo wanawake tukiendelea kufanya kazi kwa bidii mchango wetu kwa jamii
utaendelea kuonekana na kuthaminiwa na hivyo tunaweza tukawa tunapata nafasi
kubwa na nzuri ya kulitumikia taifa, hii historia ya kubaki nyuma tutaiondoa
wanawake wenyewe kwa kufanya kazi kwa bidi,” amesema.
Naye Makinda amewataka wanawake kujiamini
sambamba na kuwa na uthubutu huku akiwasihi kujitika katika utafutaji wa elimu
kwani ndiyo mkombozi wa maendeleo ya wanawake.
“Elimu ni kitu muhimu sana, wanawake wengi
elimu zao ni ndogo wananyanyasika wananyang’anywa mali sababu hawajui wanaenda
wapi, elimu yenyewe siyo ya utaniutani, wenyewe wanasoma lakini hawajui
wanasoma nini. Mkombozi wa mwanamke ni kupatikana elimu sahihi ya kuweza
kupambanua maisha yake na kujua haki zake ziko wapi na si kumdekeza sababu
ukimdekeza hatuwezi kufanya chochote,” amesema na kuongeza.
“Elimu inamfanya mwanamke athubutu, kama
huna elimu hijuamini ndiyo unatengeneza mazingira ya kupata mafanikio kwa
kupitia mtu, kusoma vizuri kujiamini, kuwa na uthubutu mwengine anataka kwenye
kazi apelekwe na mtu.”
Na Regina Mkonde
No comments:
Post a Comment