Uzinduzi
wa gereza jipya la Wilaya ya Chato unatarajia kupunguza gharama za
usafirishaji na msongamano wa wahalifu katika magereza mengine ambayo yalikuwa
yakihifadhi waalifu kutoka Wilaya hiyo.
Akizungumza
katika hafla fupi ya kuzindua wa Gereza
hilo , Waziri wa Mambo ya Ndani Dkt.Mwigulu Nchemba alisema katika Wilaya ya Chato kumekuwa na changamoto ya kutokuwa na Gereza na kulazimika kupeleka waarifu katika Gereza la Biharamulo hivyo gereza hilo litapunguza gharama za usafirishaji wa waharifu ambao wa walikuwa wakipelekwa magereza ya mbali ili kuhifadhiwa.
hilo , Waziri wa Mambo ya Ndani Dkt.Mwigulu Nchemba alisema katika Wilaya ya Chato kumekuwa na changamoto ya kutokuwa na Gereza na kulazimika kupeleka waarifu katika Gereza la Biharamulo hivyo gereza hilo litapunguza gharama za usafirishaji wa waharifu ambao wa walikuwa wakipelekwa magereza ya mbali ili kuhifadhiwa.
“
Ujenzi wa Gereza hili utasaidia kuendeshwa kwa mashitaka kwa kufuata ratiba kwa
kuwa wakati mwingine ratiba zinaingiliana lakini pia changamoto za magari,
mafuta na umbali zilikuwa kikwazo kikubwa katika uendeshaji wa mashitaka hivyo kusababisha
watu wenye matatizo mbalimbali kuendelea kushikiliwa katika magereza kwa muda
mrefu huku akikosa haki zake hata kama hana hatia”Alisema Mwigulu.
Aidha,
Dkt Mwigulu nchemba ametoa rai kwa maafisa na askari wa gereza kuhakikisha wanatunza
majengo na miundombinu ya gereza hilo na kufanya kazi kwa uadilifu ili maadili
yaliyowekwa katika magerezani yanazingatiwa .
”
licha ya kazi nzuri inayofanywa na viongozi walio wengii zipo taarifa kwenye
baadhi ya magereza watumishi hawazingatii maadili ya kazi kwa kuwa wengine
wamekuwa wakiwapa waalifu simu bila kujua wanafanya mawasiliano na watu wa
namna gani vitendo hivi vina hatarisha usalama wa gereza na askari
pia”Alisisitiza Mwigulu.
Kwa
upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi
Robert Gabriel amelitaka jeshi la magereza kupitia gereza la Wilaya ya Chato ambalo limejengwa kijiji cha Nyangomango kutumia maeneo yaliyopo na watakayopewa na Mkoa kuzalisha mazao mbalimbali ya kilimo na mifugo ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa Mkoa na taifa.Ameongeza kuwa jeshi la magereza limejijengea heshima kubwa nchini kwa kuzalisha vifaa bora kama vile samani za nyumbani na ofisini, viatu hivyo jeshi linaweza kuleta mapinduzi ya kimkakati ya kiuchumi.
Robert Gabriel amelitaka jeshi la magereza kupitia gereza la Wilaya ya Chato ambalo limejengwa kijiji cha Nyangomango kutumia maeneo yaliyopo na watakayopewa na Mkoa kuzalisha mazao mbalimbali ya kilimo na mifugo ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa Mkoa na taifa.Ameongeza kuwa jeshi la magereza limejijengea heshima kubwa nchini kwa kuzalisha vifaa bora kama vile samani za nyumbani na ofisini, viatu hivyo jeshi linaweza kuleta mapinduzi ya kimkakati ya kiuchumi.
Naye
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kagera Nehemia Nkondo ameeleza katika taarifa kuwa
ujenzi wa Gereza la Chato ulianza mwaka 2011 katika kijiji cha Nyangomango kwa
kupata hekari 50 kutoka kwa wananchi ambapo serikali ilitoa zaidi ya Shilingi
bilioni 1.5 mpaka sasa mradi umetumia kiasi cha shilingi milioni 613.6 sawa na
asilimia 40%. kiasi cha Shilingi milioni 903.6 zinaendelea kutumika ambapo kuna
ujenzi wa mabweni 4 ya wafungwa yenye uwezo wa kuhifadhi wafungwa 50 kila moja,
uvutaji wa maji na ujenzi wa mabweni 2 ya wanawake.Kazi zinazoendelea ni ujenzi
wa jengo la utawala, nyumba za watumishi.
No comments:
Post a Comment