Hii ni mara ya kwanza kwa wawili hao kukutana tangu walipotofautiana kuhusu uchaguzi mkuu uliokuwa na upinzani mkali wa Agosti 8, 2017 na wa marudio Oktoba 26 ambao Odinga alisusia.
Agenda ya kikao chao haikuwekwa wazi. Baada ya kikao chao Kenyatta na Odinga walitarajiwa kulihutubia taifa.
Seneta wa Siaya James Orengo, mshirika wa karibu wa Odinga aliliambia shirika la habari la Reuters akithibitisha kufanyika kikao hicho.
“Kinafanyika sasa, lakini tutatoa maelezo zaidi kitakapokuwa kimemalizika,” amesema.
Msemaji wa Ikulu Manoah Esipisu aliwaambia waandishi wa habari kwamba Odinga atakuwa wa kwanza kuhutubia na kisha Rais Kenyatta atatoa maoni yake.
Kikao cha viongozi hao kimefanyika siku ambayo Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Rex Tillerson anatarajiwa kuwasili Nairobi akiwa katika ziara ya Afrika.
CHANZO: MWANCHI
No comments:
Post a Comment