UJUMBE WA RAIS WA POLAND WATUMA SALAMU ZA RAIS MAFUGULI KWA WAZIRI HARRISON MWAKYEMBE

Pix 05SERIKALI ya Jamhuri ya Poland mapema mwezi April mwaka huu inatarajia kufungua upya Ofisi za Ubalozi wa nchi hiyo hapa nchini ambazo zilifungwa kwa muda, hatua inalenga kuimarisha uhusiano na ushirikiano baina ya Mataifa hayo.

Hayo yamesemwa leo Ijumaa (Februari 23, 2018) Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe wakati alipokuwa Salamu za Rais wa Poland kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

Dkt. Mwakyembe alisema hatua zote muhimu za ufunguzi wa Ubalozi huo, taratibu zote muhimu kwa ajili ya ufunguzi Ofisi za Ubalozi huo tayari zimekamilika na kuongeza kuwa kufunguliwa kwa ubalozi kutazidi kudumisha ushirikiano na urafiki wa muda mrefu baina ya Tanzania na Poland pamoja na kuimarisha diplomasia ya uchumi baina ya mataifa hayo.

“Serikali ya Jamhuri ya Poland imekuwa na ushirikiano wa muda mrefu na Tanzania, ambapo matunda ya ushirikiano ni kwa Serikali yetu kupata wa mkopo wa masharti nafuu uliofanikisha uanzishaji wa kiwanda kikubwa cha matrekta kibaha Mkoani Pwani” alisema Dkt. Mwakyekmbe.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais wa Poland Krzysztof Szczerski  alisema ziara yake ya kuja nchini ni kuwasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Poland ambapo pamoja na mambo mengine Serikali ya nchi hiyo imekusudia kuimarisha mahusiano yake ya kiuchumi na Tanzania.

Aliongeza kuwaa katika kuendeleza jitihada zake za kuimarisha uhusiano wake na Tanzania, Serikali ya Poland tayari inaendesha miradi mbalimbali ya uwekezaji nchini ambapo Rais wa Poland ameahidi kuimarisha ushirikiano huo baina yake na Rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

“Niwewasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Poland ambapo pamoja na mambo mengine, amemualika Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenda nchini Poland kwa ajili ya ziara maalum ya kiserikali” alisema Szczerski.


Share:

No comments:

SIKILIZA JAMII FM

Blog Archive

IDADI YA WASOMAJI

HABARI ZA HIVI PUNDE

HABARI KUU WIKI HII

WAENDESHA BLOG

Contact Form



Recent post