Waziri wa Maliasili na Utalii,
Dk. Hamisi Kigwangalla ameuagiza uongozi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania
TFS kujenga kituo cha ulinzi cha kudumu katika eneo la chanzo cha maji ya mto
zigi kilichopo ndani ya Hifadhi ya Mazingira Asilia Amani kwa ajili ya kulinda
chanzo hicho.
Dk. Kigwangalla ametoa agizo
hilo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea
eneo la chanzo hicho na
kukuta uharibifu mkubwa unaofanywa na baadhi ya wananchi wanaodaiwa kuchimba madini ya dhahabu katika eneo hilo la hifadhi kinyume cha sheria “Nimeagiza
watu wa TFS wajenge kituo cha ulinzi cha kudumu katika eneo hili, na waweke walinzi wetu wa kudumu hapa badala ya kutegemea kufanya patrol (doria) na kuondoka, kwasababu eneo hili wananchi wanaamini lina madini ya dhahabu kwahivo kila siku wataendelea kuja kujaribu kuvuna dhahabu kutoka hapa.
kukuta uharibifu mkubwa unaofanywa na baadhi ya wananchi wanaodaiwa kuchimba madini ya dhahabu katika eneo hilo la hifadhi kinyume cha sheria “Nimeagiza
watu wa TFS wajenge kituo cha ulinzi cha kudumu katika eneo hili, na waweke walinzi wetu wa kudumu hapa badala ya kutegemea kufanya patrol (doria) na kuondoka, kwasababu eneo hili wananchi wanaamini lina madini ya dhahabu kwahivo kila siku wataendelea kuja kujaribu kuvuna dhahabu kutoka hapa.
“Kwasababu sisi kazi yetu ni
kuhifadhi Maliasili ambayo tumepata kama urithi wa nchi yetu, niwahakikishie kwamba
tutaimarisha ulinzi kwa kuanzisha kituo cha ulinzi hapa ili askari wawe
wanabadilishana na kudhibiti kabisa uharibu ambao umekuwa ukifanyika, kwasababu maji
yanayotoka katika chanzo hiki yanakwenda kunywesha Muheza yenyewe na wilaya
wa Tanga, tukiharibu hapa yatakosekana maji safi na salama” alisema Dk.
Kigwangalla.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu
wa Wakala huyo, Prof. Dos Santos Silayo alisema pamoja na eneo hilo kwa
sasa kuwa linalindwa na askari wa Suma JKT watahakikisha ulinzi
unakuwepo muda wote kwa kutekeleza agizo hilo la Waziri la kujenga kituo cha ulinzi
cha kudumu ili askari wawepo katika eneo hilo muda wote.
“Lengo letu ni kuhakikisha kwamba
wananchi hawaingii ili tusiwe tunawashtukiza kuwakamata na kwachukulia
hatua, lazima tuwe watu wa kuzuia uhalifu usitokee, nia yetu ni kuwa na kituo
mara moja kama alivyoelekeza Mhe. Waziri na hili jambo tumelichukua kama
maelekezo na tutalitekeleza kwa nguvu kabisa,” alisema Prof. Dos Santos
Silayo.
Awali Dk. Kigwangalla
alitembelea kikundi cha wafugaji wa vipepeo katika Tarafa ya Amani ambao waliiomba
Serikali ifungulie vibali vya kusafirisha bidhaa hiyo nje ya nchi, aliahidi
kuyafanyia kazi maombi yao huku akiwataka kutumia fursa ya ufugaji huo kama bidhaa ya
utalii kuwavutia watalii wanaotembelea Hifadhi ya Mazingira Asilia Amani.
Akiwa mkoani Tanga alitembelea pia
Kituo cha Mambo ya Kale cha Mapango ya Amboni na kusema Wizara yake
itaboresha kituo hicho pamoja na vituo vingine vya Mambo ya Kale ili kupanua wigo wa vivutio
vya utalii nchini viweze kuchangia zaidi kwenye pato la Taifa.
Katika ziara hiyo ya siku moja
mkoani Tanga alitembelea pia shamba la miti ya Mitiki Longuza, Makumbusho ya
Shaban Robert na Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi.
No comments:
Post a Comment