Mvua zilizoambatana na upepo mkali zilizonyesha usiku
wa jana zimeacha athari kubwa kwa Jeshi la Polisi kwa kuharibikiwa na
jengo lao la ofisi pamoja na kujeruhiwa askari mmoja.
Akizungumza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa
Kipolisi wa Kinondoni, ACP Muliro Jumanne Muliro amekiri kutokea kwa
tukio hilo na kusema ofisi ndogo iliyopo ndani ya jengo la serikali ya Mtaa wa
Goba limeharibika kufuatia kuangukiwa na nguzo ya mnara wa simu kuangukia.
"Askari mmoja amejeruhiwa katika
ajali hiyo ila alifanikiwa kukimbizwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili kwa
matibabu", amesema Kamanda Muliro.
Mbali na tukio hilo, mvua zilizonyesha
usiku wa jana (Machi 07, 2018) zimeweza kuwaathiri pia baadhi ya jamii kwa
kuezua paa za nyumba zao na kusababisha kukosa makazi.
No comments:
Post a Comment