
PALANGO amebainisha hatua hizo za kinidhamu kuwa ni pamoja na
kuwapa barua za kujieleza wafanyakazi hao, za kwanini hatua za kinidhamu
zisichukuliwe dhidi yao.
Katika hatua nyingine Katibu tawala huyo kijana machachari pindi
awapo kazini, amemuagiza Mratibu Elimu KATA kuhakikisha MCHAKAMCHAKA kwa wanafunzi
unarudishwa kama zilivyo taratibu za kawaida .
“Wanafunzi wamenithibitishia Kuwa hawakimbii tena mchakamchaka,
ambao ni muhimu kwa ukuaji wa Afya ya mwili na akili zao na hivyo kuimarisha
taaluma zao, mratibu hakikisha mchakamchaka unarudi kama kawaida” amesema PALANGO
Ni utamaduni wa Wilaya ya NANYUMBU kufanya Mzunguko wa Mazoezi
katika Kila Kata za Wilaya hiyo na Mwezi huu ilikuwa ni Zamu ya KATA ya LIKOKONA.
Mazoezi hayo yamehudhuriwa na wakuu wa Idara, Wananchi, DIWANI
wa KATA, Kaimu Mkurugenzi,Walimu na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari LIKOKONA na
Shule mbili za Msingi na Mgeni rasmi alikuwa ni Katibu Tawala Wilaya SALUM
PALANGO, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo Wilaya na Katibu
wake ni Afisa Utamaduni/ Afisa Michezo wa Wilaya.
No comments:
Post a Comment